Thursday 24 December 2015

Tangazo la Nafasi za Masomo kwa watoto wa miaka 2-5 Morogoro Mjini


 Je unatafuta shule kwa ajili ya mwanao wa miaka 2-5?


 Je unahitaji kufanya shughuli zako za uzalishaji mali huku mwanao akiwa katika mikono salama  ya walimu wazoefu kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa nane ama saa kumi jioni?


Je unahitaji mwanao ajifunze maadili mema na nidhamu?


Je unatafuta shule yenye ada nafuu huku mwanao akipata huduma zote muhimu? Kama chakula, maji safi na salama, na kupumzika (kulala) baada chakula cha mchana?



Je unahitaji mwanao ajifunze, kuongea,kusoma, kuandika na kuhesabu kwa ufasaha katika lugha lugha zote mbili kingereza na Kiswahili?


Je unahitahi mwanao apate huduma za kiasikolojia kutoka kwa mtaalamu  mwenye uzoefu wa saikolojia mwenye shahada ya uzamili ya chuo kikuu cha Dar es salaam?



Happy valley day care center  ndiyo jibu lako. Tunapatikana boma road karibu na ofisi ya mkuu wa mkoa wa Morogoro

Wahi sasa  nafasi ni chache fomu bado zinapatikana, shule itafunguliwa 18/1/2016. 

Kwa maelezo zaidi wapigie simu namba 0714 022 038 au 0783 400 701

Mandhari ya Happy Day Care Center


Happy Valley Day Center ipo eneo lenye utulivu sana linalofaa kwa malezi ya watoto
Mandhari tulivu kabisa inayofaa kwa michezo ya watoto

Kuta za bustani zinapendeza na zinamaandishi kwa ajili ya watoto kujifunza wakiwa nje ya darasa

Sehemu ya jengo la Happy Valley Day Care Center



Lango kuu la kuingilia Happy Valley Day Care Center


Thursday 19 November 2015

TANGAZO LA NAFASI YA KAZI - (Re-Advertised)




Tupo karibu na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Plot No. 214, Boma Road
P.o. Box 4664 Morogoro, TANZANIA.

Simu: 0783400701 ama
0714022038

Email: Happyvalleyschools@gmail.com



TANGAZO LA NAFASI YA KAZI

Happy Valley Day Care Center iliyopo Morogoro mjini karibu na ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro inatangaza nafasi (1) ya kazi ya mwalimu wa elimu ya awali.


Majukumu ya mwalimu wa awali yatakuwa yafuatayo
· Kuwapokea watoto wafikapo shule na kuhakikisha wamerudi salama majumbani mwao
· Kuwafundisha watoto elimu ya awali
· Kuwahudumia watoto katika mahitaji yao mbalimbali
· Kuandaa michezo ya watoto na kuwasimamia wanapocheza
· Kutoa taarifa za watoto kwa wazazi kupitia shajara /diary za watoto
· Kuhakikisha usalama wa watoto wakati wote
· Kuhakikisha usafi wa watoto wakati wote
· Kuandaa ripoti za mitihani za watoto.
· Kufanya kazi nyingine yoyote ile inayoendana na taaluma ya elimu ya awali atakayoelekezwa na mkuu wake wa kazi.

Sifa za Muombaji
Awe anapenda watoto
Awe angalau na cheti cha ualimu wa elimu ya awali kutoka chuo kinachotambulika
Awe na uwezo wa kuongea na kuandika kwa ufasaha lugha ya Kiingereza na Kiswahili
Awe na umri usiopungua miaka (25)
Awe mbunifu katika kuandaa michezo ya watoto
Awe na ujuzi wa kuwaelewa watoto kwa haraka
Awe na uwezo wa kujituma kuliko kuamrishwa

Mwenye uzoefu wa kufundisha watoto atapewa kipaumbele


Tuma maombi yako kupitia anwani ya barua pepe (Email) inayoonekana hapo juu. Pamoja na barua yako ya maombi, ambatanisha wasifu wako (CV)  na nakala za vyeti vyako. Mwisho wa kutuma maombi ni tar 10/12/2015.

Kwa maelezo zaidi piga kupitia namba za simu zinaonekana hapo juu.

Friday 11 September 2015

Are you based in Morogoro? Looking for a child care center for your kid? Please read this post

Do you have a kid with the right age to join child care center?  Do you have a child aged 2 to 5? Are you based in Morogoro Town? Are you residing in Boma, area 6, Kihonda, Kichangani, Msamvu, Forest, Nanenane, or any area relatively close to the offices of the Morogoro Regional Commissioner?

Are you looking for the right school for your child? The school you can trust in the provision of ultimate care and learning to your child? The school that guarantees safety to your child? The school that provides recommended sports and games to your child? Quality food?

Do you need your child to master in being self confident, being considerate, industrious, hardworking and self learning?

Do you need to be sure that your child is left in good hands the whole day while you are at work? Are you looking for teachers who will treat your child as their friend? Are you also looking for teachers who want to be friends with every parent of the kid at school?

Do you need your child to feel at home while at school?

Do you need your child be taught by God fearing teachers?

If you have answered yes to any of the above questions then your choice is Happy Valley Day Care Center. Happy Valley Day Care Center is a new school with experienced teachers.  The school is located in Boma area close to the offices of Morogoro Regional Commissioner in  Morogoro town and is now recruiting students for January 2016 intake.

Please contact us at happyvalleyschools@gmail.com

Unaishi Morogoro? Unatafuta shule ya awali kwa ajili ya mwanao? Soma hapa tafadhali

Una mwanao mwenye umri wa miaka miwili hadi sita? Unaishi Morogoro maeneo ya Area 5, Area 6, Kihonda, Kichangani, Msamvu, Nanenane ama eneo jingine lolote la Morogoro?

Unatafuta shule kwa ajili ya mwanao? Shule inayoaminika kwa malezi bora ya mtoto wako? Usalama wa mtoto akiwa shuleni? Chakula bora? Michezo bora?

Unahitaji mwanao ajengewe uwezo wa kujiamini, utu wema, uchapa kazi, kujitegemea, kupenda kujifunza na kadhalika?

Unahitaji kumwacha mwanao akiwa kwenye mikono ya walezi unaowaamini ambao wanataka kujenga urafiki kati yako, wao na mwanao?

Unahitaji mtoto wako awe shuleni lakini ajisikie yupo nyumbani?

Unahitaji mtoto wako afundishwe na walimu wenye hofu ya Mungu?

Kama umejibu ndiyo kwenye moja ya maswali hapo juu basi Happy Valley Day Care Center ni chaguo lako. Happy Valley Day Care Center ni shule mpya yenye walimu wazoefu iliyopo eneo la Boma karibu na ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Morogoro .  Shule hii inakaribisha watoto wenye miaka miwili hadi mitano wajiandikishe tayari kwa muhula wa masomo utakaoanza Januari 2016.

Kwa mawasiliano zaidi tuandikie
Happyvalleyschools@gmail.com